Msafara wa wachezaji, benchi la ufundi, baadhi ya viongozi wa klabu ukiongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ambaye pia ni Mwenyekiti Kamati ya Mashindano, Ahmed Mgoyi umewasili salama mjini Algiers, Algeria na kupokelewa na Balozi wa Tanzania wa Algeria, Omary Mzee. #NguvuMoja