YANGA: Yaingia Kambini Kuiwinda KMC

Kikosi cha vinara wa ligi kuu ya Tanzania Bara Yanga kinaingia kambini leo katika Hotel ya Nefaland kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya KMC

Mchezo huo utapigwa keshokutwa Jumapili, March 10 2019 saa kumi kamili jioni katika uwanja wa Taifa

Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema wachezaji 20 wanatarajiwa kuingia kambini leo jioni kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo huo

Tangu irejee kutoka Mwanza ambako iliichapa Alliance Fc bao 1-0, Yanga imekuwa ikijifua kwenye uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar es salaam