Mchezo huo utapigwa keshokutwa Jumapili, March 10 2019 saa kumi kamili jioni katika uwanja wa Taifa
Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema wachezaji 20 wanatarajiwa kuingia kambini leo jioni kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo huo
Tangu irejee kutoka Mwanza ambako iliichapa Alliance Fc bao 1-0, Yanga imekuwa ikijifua kwenye uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar es salaam