Kabwili augua Yanga ikijiandaa kuikabili KMC

Kesho Jumapili kikosi cha Yanga kitashuka dimba la Taifa kuikabili KMC katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara unaotarajiwa kuanza saa kumi kamili jioni

Katika mchezo wa kesho Yanga itakosa huduma ya mlinda lango wake kinda Ramadhani Kabwili ambaye ni mgonjwa

Hata hivyo, mkufunzi wa makipa Juma Pondamali amesema hana wasiwasi na kusokena kwa Kabwili kwa kuwa Kindoki na Hamid wapo

Yanga itaingia kwenye mchezo wa kesho ikiwa na kumbukumbu ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 kwenye mchezo wa mzunguuko wa kwanza, bao lililowekwa kimiani na Feisal Salum ‘Fei Toto’ kwa mkwaju wa adhabu kwenye dakika za lala salama

Ligi Kuu ya Tanzania Bara inaendelea leo kwa michezo minne kupigwa kwenye viwanja mbalimbali