FT : JS Saoura 2-0 Simba

Simba imepoteza mchezo wake wa tatu ugenini baada ya kufungwa mabao 2-0 na JS Saoura katika mchezo wa ligi ya mabingwa raundi ya tano uliopigwa nchini Algeria

Wenyeji waliutawala mchezo huo, ushindi ni matokeo yanayoakisi walichokifanya katika dimba lao la nyumbani

Licha ya kufungwa vijana wa Patrick Aussems walionekana kuimarika ukilinganisha na michezo mingine miwili ya ugenini ambayo waliruhusu mabao 10

Matokeo hayo yameishusha Simba mpaka nafasi ya nne kwenye msimamo wa kundi D wakibaki na alama zao sita

JS Saoura wamechupa mpaka nafasi ya kwanza baada ya kufikisha alama nane

Al Ahly inashika nafasi ya pili ikiwa na alama saba sawa na Vita Club inayoshika nafasi ya tatu Al Ahly ikifaidika na matokeo baina ya timu hizo

Mapema leo Vita Club iliilaza Al Ahly bao 1-0 wakati Al Ahly ilishinda mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa Misri

Simba sasa ni lazima ishinde mchezo wa mwisho dhidi ya Vita Club, mchezo ambao utapigwa Jumamosi ijayo kwenye uwanja wa Taifa

Kimahesabu bado Simba ina nafasi ya kutinga robo fainali