
Wenyeji waliutawala mchezo huo, ushindi ni matokeo yanayoakisi walichokifanya katika dimba lao la nyumbani
Licha ya kufungwa vijana wa Patrick Aussems walionekana kuimarika ukilinganisha na michezo mingine miwili ya ugenini ambayo waliruhusu mabao 10
Matokeo hayo yameishusha Simba mpaka nafasi ya nne kwenye msimamo wa kundi D wakibaki na alama zao sita
JS Saoura wamechupa mpaka nafasi ya kwanza baada ya kufikisha alama nane
Al Ahly inashika nafasi ya pili ikiwa na alama saba sawa na Vita Club inayoshika nafasi ya tatu Al Ahly ikifaidika na matokeo baina ya timu hizo
Mapema leo Vita Club iliilaza Al Ahly bao 1-0 wakati Al Ahly ilishinda mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa Misri
Simba sasa ni lazima ishinde mchezo wa mwisho dhidi ya Vita Club, mchezo ambao utapigwa Jumamosi ijayo kwenye uwanja wa Taifa
Kimahesabu bado Simba ina nafasi ya kutinga robo fainali