Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, Mo amesema kwa sasa hapendi kuzungumza maneno mengi lakini anawaita uwanja wa Taifa mashabiki wa Simba Watanzania wote kuiunga mkono Simba katika mchezo huo muhimu
“Sina maneno mengi, tukutane uwanjani wanaSimba na waTanzania wote kwa ujumla,” ameandika Mo
Katika michezo yote msimu huu ambayo Mo yuko uwanjani, Simba imeibuka na ushindi.
Licha ya kuwa mwekezaji, Mo amejipambanua kuwa shabiki na muhamasishaji namba moja wa klabu ya Simba kuelekea ‘gemu’ kubwa