Okwi, Nyoni wanogesha mazoezi Simba

Kiraka Erasto Nyoni na mshambuliaji Emmanuel Okwi leo walikuwepo uwanjani wakijifua na kikosi cha Simba kinachojiandaa na mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya AS Vita takaopigwa Jumamosi, March 16 katika uwanja wa Taifa

Simba iliyorejea jana kutoka Algeria inajifua kwenye uwanja wa Boko Veterans

Nyoni na Okwi hawakusafiri na Simba ilipokwenda nchini Algeria kumenyana na JS Saoura kutokana na kuwa majeruhi

Wachezaji hao leo wamejumuika na wachezaji wengine wakihusika katika program zote za mazoezi hivyo kuongeza matumaini kuwa wako tayari kwa ajili ya mchezo wa Jumamosi