
Vita Club ilikubali kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Simba na kuondoshwa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika ikiiacha Simba ikitinga robo fainali
Akizungumza baada ya mchezo jana, Ibenge alisema Simba ina wachezaji wazuri
Aidha, Ibenge alifichua kuwa walimuwekea ulinzi mkali Meddie Kagere kwa kuwa ndio mchezaji waliokuwa wakimuhofia zaidi
“Simba walionyesha ushindani mkali kwetu, walicheza vizuri matokeo waliyopata walistahili, tunawapongeza,” amesema
“Kagere ndio mchezaji tuliyekuwa tunamuhofia zaidi na niliwaagiza wachezaji wangu wamchunge lakini mwisho wa siku mpira ni mchezo wa makosa, tumefanya makosa tumeadhibiwa”
Mabao ya Simba yalifungwa na Mohammed Hussein na Clatous Chama aliyefunga bao la ushindi katika dakika za lala salama