SIMBA vs RUVU SHOOTING

Baada ya juzi kuitoa Tanzania kimasomaso kwa kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika, kikosi cha Simba kesho Jumanne kitakuwa dimba la Taifa kuikabili Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa saa moja jioni

Simba inashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama 51

Hata hivyo ina michezo tisa ya viporo hivyo kuwa na nafasi kubwa ya kutetea ubingwa wake kama itashinda yote