
Aussems ametoa tahadhari hiyo hasa ikizingatiwa kwenye kikosi cha Stars Simba ina wachezaji wanne
Wachezaji wa Simba walioitwa kikosi cha Stars ni Aishi Manula, Jonas Mkude, John Bocco na Erasto Nyon
Ikumbukwe mwishoni mwa mwaka jana Simba ilimpoteza beki wake Shomari Kapombe ambaye yuko nje kwa zaidi ya miezi mitano akiuguza majeraha aliyopata akiwa katika kambi ya Stars Afrika Kusini
Simba inakabiliwa na michezo ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa, droo ya hatua hiyo ikiatarajiwa kufanyika nchini Misri kesho
Kocha Mkuu wa Stars Emannel Amunike ameanza kukinoa kikosi cha Stars jana, wachezaji wakifanya mazoezi mara mbili kwa siku
Stars inajiandaa kuikabili Uganda Jumapili, March 24 2019