Aussems alia na mazoezi ya Stars

Kocha Mkuu wa timu ya Simba Patrick Aussems ameingiwa na hofu kutokana mazoezi wanayopewa wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kuwa yanaweza kupelekea majeruhi

Aussems ametoa tahadhari hiyo hasa ikizingatiwa kwenye kikosi cha Stars Simba ina wachezaji wanne

Wachezaji wa Simba walioitwa kikosi cha Stars ni Aishi Manula, Jonas Mkude, John Bocco na Erasto Nyon

Ikumbukwe mwishoni mwa mwaka jana Simba ilimpoteza beki wake Shomari Kapombe ambaye yuko nje kwa zaidi ya miezi mitano akiuguza majeraha aliyopata akiwa katika kambi ya Stars Afrika Kusini

Simba inakabiliwa na michezo ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa, droo ya hatua hiyo ikiatarajiwa kufanyika nchini Misri kesho

Kocha Mkuu wa Stars Emannel Amunike ameanza kukinoa kikosi cha Stars jana, wachezaji wakifanya mazoezi mara mbili kwa siku

Stars inajiandaa kuikabili Uganda Jumapili, March 24 2019