
Katika mchezo huo utakaopigwa saa moja jioni, Simba itawakosa baadhi ya nyota wake ambao wameitwa kujiunga na timu za Taifa
Nahodha John Bocco, Jonas Mkude, Erasto Nyoni na Aishi Manula wameitwa katika kikosi cha timu ya Taifa kinachojiandaa na mchezo dhidi ya Uganda Cranes utakaopigwa mwishoni mwa wiki
Meddie Kagere ameitwa kikosi cha Rwanda wakati Emannuel Okwi na Juuko Murshid wao wameitwa kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema atafanya mabadiliko madogo ya kikosi chake kitakachoshuka dimbani leo
Amewatoa wasiwasi Wanamsimbazi kuwa watafanya vizuri katika mchezo huo lengo likiwa ni kuondoka na alama zote tatu