Mpinzani wa Simba robo fainali ligi ya mabingwa kujulikana leo

Droo ya hatua ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika inafanyika leo huko Misri

Simba ikiwa miongoni mwa timu nane zilizotinga hatua hiyo, baadae leo itaweza kumfahamu mpinzani wake kati ya Esperance ya Tunisia, Wydad Casablanca ya Morocco, TP Mazembe ya Congo, Mamelodi ya Afrika Kusini, Horoya ya Guinea, Asec Mimosa ya Ivory Coast na Al Ahly ya Misri.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Simba Crescentius Magori na Mwenyekiti wa klabu hiyo Swedi Mkwabi wataiwakilisha Simba katika droo hiyo inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchini

Kuelekea droo hiyo, kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema baada ya kufanikiwa kutinga robo fainali, hawaihofii timu yoyote watakayopangwa nayo katika hatua inayofuata

Michezo ya duru ya kwanza ya hatua ya robo fainali itapigwa April 05 2019 huku michezo ya marudiano ikitarajiwa kupigwa April 12