YANGA : MICHANGO

Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya Yanga Mh Anthony Mavunde amesema nahodha Ibrahim Ajib na Kocha Mwinyi Zahera hawajaondolewa kutia saini katika Akaunti Maalum iliyofunguliwa kukusanya fedha kwa ajili ya kuboresha kikosi cha timu hiyo

Mavunde ameiambia Yanga TV kuwa Ajib na Zahera watabaki kuwa watia saini kutokana na umuhimu wao

“Lazima kapteni na kocha waendelee kubaki kuwa watia saini sababu hawa ni watu muhimu sana,” amesema Mavunde

Aidha ili kuongeza uaminifu na kuwahakikishia Wanayanga kuwa fedha wanazochangia ziko salama, Mavunde amesema Kamati imependekeza kuongeza watia saini wengine ambao ni Mhasibu wa klabu na kiongozi mmoja wa Yanga

Pia Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Kamati maalum ambao ndio wanaongoza zoezi la kutafuta fedha nao watakuwa miongoni mwa watia saini

“Lakini pia viongozi waliopo, kwa maana mtaalamu wetu ambaye ni mhasibu na kiongozi mmoja wa Yanga nao watakuwepo sehemu ya watia saini”

“La tatu ni kundi la Kamati yenyewe ambao kimsingi ndio watafuta fedha, Mwenyekiti nitakuwepo miongoni mwa watia saini na Makamu Mwenyekiti”

“Hii yote tunaifanya katika kuongeza uwajibikaji na vilevile tuishi kwenye misingi ya uadilifu mkubwa ili fedha inayochangwa na Mwanayanga iende kufanya kazi iliyokusudiwa”