Ngasa ashikiria rekodi ya michezo, mabao Stars

Wakati Watanzania wakiusubiri kwa hamu mchezo wa Stars dhidi ya Uganda utakaopigwa keshokutwa Jumapili katika uwanja wa Taifa, winga wa Yanga Mrisho Ngasa ‘Uncle’ ni miongoni mwa wachezaji wenye historia ya kipekee katika kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania

Ngasa ameichezea Stars michezo 100 na kufanikiwa kufunga mabao 25. Bado rekodi yake hiyo ya michezo na mabao haijavunjwa

Ngasa mwenye umri wa miaka 29 anasema bado hajastaafu kuichezea timu ya Taifa na yuko tayari kuitumikia iwapo ataitwa siku zijazo

“Bado sijatangaza kustaafu kuichezea Stars, bado naamini ninayo nafasi ya kucheza na kuonyesha uwezo kama ilivyokuwa mwanzo,” amesema Ngasa

“Sijakata tamaa nitapambana kuhakikisha wakati wmingine napata nafasi ya kulitumikia taifa langu muda bado ninao na kipaji kipo kwanini nisiitwe hakuna raha kama kucheza katika timu ya taifa”

Ngasa amekuwa na msimu mzuri katika kikosi cha Yanga akijihakikishia namba kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Mwinyi Zahera

Ngasa ameifungia Yanga mabao manne katika ligi kuu ya Tanzania Bara