
Mo amesema Watanzania wote tunapaswa kuwa wamoja kuelekea mchezo huo ambao Stars inahitaji kushinda ili iweze kukata tiketi ya kutinga fainali za michuano ya AFCON 2019 itakayofanyika nchini Misri baada ya kukosa michuano hiyo kwa miaka
39
Mo amewahakikishia wachezaji wa Stars kuwa Watanzania wote wako nao kwani wanashauku ya kuiona timu yao ikifuzu kwa fainali za michuano hiyo, hivyo wasiwaangushe
“Watanzania wote tupo nyuma yenu wachezaji wetu wa Taifa Stars kuhakikisha tunashinda dhidi ya Uganda, sababu zote za kufanya hivyo tunazo,” amesema
“Naamini mtashinda na kutufanya Watanzania tutembee kifua mbele. Nawaombea kwa Mwenyezi Mungu mfanye”
Kuelekea mchezo huo utakaopigwa keshokutwa Jumapili saa 12 jioni katika dimba la Taifa, mashabiki wametakiwa kujitokeza kwa wingi ili kuwapa sapoti wachezaji
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Kassim Majaliwa atakuwa mgeni rasmi katika mchezo huo ambao kiingilio ni Tsh 2000/- tu