Uganda Cranes kuwasili leo

Kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda ‘Uganda Cranes’ kinatarajiwa kuwasili leo tayari kwa mchezo dhidi ya Taifa Stars utakaopigwa kwenye uwanja wa Taifa kesho Jumapili

Mchezo huo wa kukamilisha ratiba ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za AFCON 2019, unatarajiwa kuanza saa 12 jioni

Uganda ambayo tayari imeshafuzu kushiriki fainali hizo zitakazopigwa nchini Misri mwezi Juni ikiwa kinara wa kundi L, iliweka kambi ya wiki moja jijini Cairo

Kikosi cha timu hiyo kitakachowasili leo, kinajumuisha wachezaji wawili wa Simba, Emmanuel Okwi na Juuko Murshid