Taifa STARS : Kupewa Mamilioni Wakiifunga UGANDA | TAIFA

Mwenyekiti wa Kamati ya Saidia Taifa Stars Ishinde ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kamati yake itatoa shilingi. milioni 10 kwa kila mchezaji wa timu hiyo iwapo timu itafuzu kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika #AFCON2019

Makonda amesema Watanzania wanachokijua kwa sasa ni kwamba AFCON 2019 ni zamu yao, hivyo amewaomba wachezaji wa timu ya Taifa wahakikishe wanawapa furaha kwa kuifunga timu ya Taifa ya Uganda na kwamba wananchi wengi wamehamasika kwenda kuwashangilia.
#zamuyetuafcon2019πŸ‡ΉπŸ‡Ώ