Nitakuwepo uwanjani kuiunga mkono Stars – Tshabalala

Nahodha Msaidizi wa kikosi cha mabingwa wa soka Tanzania Bara, Simba, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ amesema ataungana na mashabiki wa soka nchini kwenda uwanjani kesho kuiunga mkono Stars itakapokuwa ikichuana na Uganda Cranes

Tshabalala amesema anaamini kikosi kilichochaguliwa na kocha Emmanuel Amunike ni kizuri na kitaweza kuipa Tanzania matokeo inayohitaji ili iweze kufuzu kwa fainali za AFCON 2019

“Nitakuwepo uwanjani kesho kuwasapoti ndugu zangu, marafiki zangu, kaka zangu kuwapa hamasa ili waweze kupata matokeo chanya katika mchezo huo”

Tshabalala amewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa kesho kuhakikisha lengo la kushinda mchezo huo linafanikishwa

Mchezo dhidi ya Uganda umepewa hamasa ya kipekee na wadau wa nyanja zote nchini kutokana na umuhimu wake

Baada ya kukosa kushiriki fainali za AFCON kwa miaka 39, Stars inaweza kupata nafasi ya kushiriki fainali hizo mwaka huu zitakazofanyika nchini Misri kama itaweza kuifunga Uganda