Rais Magufuli awaita wachezaji Stars Ikulu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli amewaalika Ikulu wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ pamoja na Bondia Hassani Mwakinyo aliyemtwanga Muargentina Sergio Eduardo katika pambano lililofanyika juzi nchini Kenya

Kulingana na taarifa iliyotolewa mapema leo na msemaji wa Ikulu Gerson Msigwa, Rais Magufuli atatoa pongezi kwao na kula nao chakula cha mchana

Jana Stars ilifanikiwa kufuzu fainali za AFCON 2019 baada ya kusubiri kwa miaka 39 ikiibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Uganda katika mchezo uliopigwa uwanja wa Taifa