Stars yakata tiketi AFCON 2019 baada ya kuichapa Uganda 3-0

Historia imeandikwa leo katika dimba la Taifa baada ya timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kufuzu kwa fainali za AFCON 2019 kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Uganda

Stars imefuzu kwa fainali hizo baada ya kusubiri kwa miaka 39

Matokeo ya suluhu ya bila kufungana kati ya Cape Verde dhidi ya Lesotho yameinufaisha Tanzania kuweza kuwa miongoni mwa timu 24 zitakazochuana nchini Misri mwezi Juni

Stars iliyokuwa katika kiwango bora, iliandika bao la kuongoza kwenye dakika ya 21 kupitia kwa Saimon Msuva aliyemalizia pasi murua ya John Bocco

Erasto Nyoni akaifungia Stars bao la pili kupitia mkwaju wa penati kwenye dakika ya 50 baada ya Samatta kumnawisha mlinzi wa Uganda ndani ya eneo la hatari

Bao lililoizamisha Uganda liliwekwa kimiani na Aggrey Morisi kwenye dakika ya 56 akimalizia krosi iliyochongwa na John Bocco

Ushindi wa Stars ulinogeshwa na idadi kubwa ya mashabiki waliofurika kuujaza uwanja wa Taifa

Kikosi cha Stars kilichoandika historia leo;

Manula, Hassan Kessy, Gadiel Michael, Agrey Morris, Kelvin Yondani, Erasto Nyoni , Saimon Msuva, Mudathir Yahya, John Bocco, Mbwana Samatta, Farid Mussa

AKIBA
Metacha Munata, Aron Kalambo, Ally Sonso, Kennedy Juma, Jonas Mkude, Himid Mao, Feisal Salum Fei Toto, Shiza Kichuya, Yahya Zaydi, Thomas Ulimwengu, Rashid Mandawa, ShabaanIddi Chilunda