
Meneja wa Simba Patrick Reyemamu amesema wanatarajia kuweka kambi ya mkoani Morogoro kujiandaa na mchezo dhidi ya TP Mazembe
Aidha Simba imechagua kutumia uwanja wa Jamhuri kwa ajili ya michezo yake ya nyumbani wakati ambao uwanja wa Taifa utakuwa umefungwa kupisha michuano ya AFCON kwa vijana inayoanza April 14-28 2019
Kwa sasa Simba inafanya mazoezi uwanja wa Boko Veterans ambapo wachezaji waliokuwa na majukumu katika timu za Taifa wanatarajiwa kuanza kuwasili kesho