Simba kwenda Morogoro Ijumaa, kuivaa Mbao Fc Jamhuri Stadium

Mchezo wa ligi kuu kati ya Simba dhidi ya Mbao Fc utapigwa kwenye dimba la Jamhuri Jumapili, March 31 2019 ambapo kikosi cha Simba kinatarajiwa kuelekea mkoani Morogoro Ijumaa ya wiki hii

Meneja wa Simba Patrick Reyemamu amesema wanatarajia kuweka kambi ya mkoani Morogoro kujiandaa na mchezo dhidi ya TP Mazembe

Aidha Simba imechagua kutumia uwanja wa Jamhuri kwa ajili ya michezo yake ya nyumbani wakati ambao uwanja wa Taifa utakuwa umefungwa kupisha michuano ya AFCON kwa vijana inayoanza April 14-28 2019

Kwa sasa Simba inafanya mazoezi uwanja wa Boko Veterans ambapo wachezaji waliokuwa na majukumu katika timu za Taifa wanatarajiwa kuanza kuwasili kesho