Dida anolewa kuibeba Simba mchezo dhidi ya Mbao Fc

Mlinda lango namba moja wa Simba Aishi Manula alipata majeraha ya kiganja cha mkono wakati akiitumikia timu ya Taifa kwenye mchezo dhidi ya Uganda

Licha ya kuhudhuria mazoezi ya Simba leo, Manula bado anaonekana hayuko vizuri, ambapo benchi la ufundi limelazimika kumuandaa kikamilifu golikipa namba mbili Deo Munishi ‘Dida’ kuelekea mchezo dhidi ya Mbao Fc

Baada ya mlinda lango kinda Ali Salim kuitwa katika kikosi cha timu ya Taifa U20, Simba imebaki na walinda lango wawili wa kikosi cha kwanza Manula na Dida

Hakuna uhakika kama Manula atakuwa ‘fit’ kabla ya Jumapili lakini huenda Simba ikalazimika kuongeza mlinda lango mwingine kutoka kikosi cha pili kuelekea mchezo wa Jumapili