
Zahera ambaye yuko Mwanza na kikosi cha Yanga ambacho leo kinatarajiwa kushuka uwanja wa CCM Kirumba kuumana na Alliance Fc katika mchezo wa robo fainali kombe la FA, amesema hana wasiwasi kama wachezaji hao wataondoka kwa kuwa amedhamiria kuisuka upya Yanga kwa ajili ya msimu ujao
Aidha Zahera amesema Yanga ya sasa sio tegemezi, haiwezi kutetereka kama wachezaji hao wataondoka hata leo
“Watu wananipigia simu kuniuliza kuhusu wachezaji wa Yanga hasa Yondani, Tshishimbi, Ajibu na Feisal kutakiwa na timu nyingine.”
“Tangu mwanzo wa ligi ukiangalia kuna mechi mingi tulizocheza, angalia mechi ngapi tuilicheza bila Kevin ngapi tulicheza bila Tshishimbi bila Ajibu na Feisal. Kuna mechi tulicheza bila watatu kati yao ndani ya mechi moja na tulishinda,” amesema Zahera
“Nikisikia leo Yanga hakuna mchezaji hata mmoja kwenye timu ninaweza kulia lakini mchezaji mmoja akikosa siwezi kukosa usingizi.”
“Mchezaji yeyote anayetaka kuondoka anaweza kuondoka, hakuna hata mchezaji mmoja anaweza kuniogopesha kwakuwa timu fulani inamtaka lakini najua msimu ujao wa ligi timu hii itabadilika sana.”
“Yanga sio team ya mchezo, Yanga ni timu kubwa na inawachezaji wakubwa. Yanga ina wachezaji wazuri lakini msimu unaokuja nadhani Yanga itakuwa na wachezaji wakubwa saana.”