Mazembe yatua nchini, yapitia Mbeya

Wapinzani wa Simba robo fainali ligi ya mabingwa barani Afrika, TP Mazembe wamewasili leo tayari kwa mchezo huo utakaopigwa Jumamosi April 06 kwenye uwanja wa Taifa

Mazembe imekuja nchini kwa kutumia ndege binafsi ambapo timu hiyo kabla ya kuja jijini Dar es salaam ilitua kwa muda mkoani Mbeya

Simba leo ilitarajiwa kucheza na JKT Tanzania mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara.

Hata hivyo mchezo huo uliahirishwa baada ya mvua kubwa iliyonyesha mapema mkoani Morogoro kujaza maji kwenye uwanja wa Jamhuri

Simba sasa inaelekeza nguvu zake kuelekea mchezo dhidi ya TP Mazembe