TP Mazembe yaingia mchecheto kuikabili Simba

Ni kama TP Mazembe imeingiwa hofu kuelekea mchezo wa Jumamosi baada ya timu hiyo kukataa kutumia basi walilopewa na Simba

Aidha timu hiyo imetoa tuhuma lukuki ikidai haitasita kupeleka malalamiko CAF kama itafanyiwa matendo yasiyo ya kiungwana

Uongozi wa timu hiyo umedai kuwa na taarifa za matukio zilizofanyiwa timu zilizokuja kucheza na Simba jijini Dar es salaam

Hata hivyo Afisa Habari wa Simba Haji Manara ameitaka timu hiyo isianze kutoa visingizio mapema na badala yake wakacheze mpira uwanja wa Taifa

Manara amesema baadhi ya timu zinajiona kuwa na haki ya kushinda zaidi kuliko timu nyingine jambo ambalo sio sahihi

Simba tayari imerejea jijini Dar es salaam kufanya maandalizi ya mwisho kuelekea mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchin