Mazoezi ya mwisho kabla ya kuivaa TP Mazembe

Kikosi cha Simba leo jioni kimefanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa Boko Veterans kabla ya kuikabili TP Mazembe kesho Jumamosi katika mchezo wa robo fainali michuano ya ligi ya mabingwa

Katika mazoezi hayo yaliyosimamiwa na kocha Patrick Aussems, ari ya wachezaji imeonekana kuwa juu, wakionyesha utayari wa mchezo huo