FT : Simba 0-0 TP Mazembe

Mchezo wa kwanza wa robo fainali ligi ya mabingwa kati ya Simba dhidi ya TP Mazembe umemalizika kwa suluhu ya bila kufungana

Mchezo huo uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa, ulishuhudiwa na malfu ya mashabiki walioongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamis Kigwangala

Simba itajilaumu yenyewe kwa kushindwa kuibuka na ushindi licha ya kutengeneza nafasi nyingi hasa kwenye kipindi cha pili

Haikuwa siku nzuri kwa nahodha John Bocco ambaye alikosa mkwaju wa penati pamoja na nafasi nyingine mbili

Simba italazimika kupata matokeo ugenini ili kuweza kufuzu nusu fainali