
Horoya ililazimishwa suluhu ya bila kufungana na Wydad Casablanca kama ilivyokuwa kwa Simba dhidi ya TP Mazembe
CS Constantine ilikubali kipigo cha mabao 3-2 nyumbani dhidi ya mabingwa watetezi Esperance
Michezo ya marudiano inatarajiwa kupigwa wiki ijayo April 13
Wawakilishi wa Tanzania, Simba watasafiri Lubumbashi DR Congo kuikabili TP Mazembe itakayokuwa nyumbani
Kwenye mchezo huo wa marudiano Simba inahitaji matokeo ya aina mbili ili iweze kutinga nusu fainali
Ushindi au sare yoyote ya mabao itaihakikishia Simba kuingia nusu fainali
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wanao uwezo wa kufuzu ugenini baada ya kufanya tathmini ya mchezo wa jana
Amesema watajipanga wakapambane ugenini kuhakikisha wanapata matokeo yanayoweza kuwapeleka hatua ya nusu fainali