Simba kuifuata TP Mazembe Alhamisi ijayo

Kikosi cha Simba kitaondoka jijini Dar es salaam Alfajiri ya Alhamisi, April 11 2019 kuelekea DR Congo tayari kwa mchezo wa marudiano, robo fainali ya ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe


Uongozi wa Simba umewaalika wapenzi, mashabiki na wanachama wa timu hiyo ambao wangependa kusafiri na kikosi cha Simba nchini Congo, kujiandikisha