Wawa nje wiki moja

Beki kisiki wa Simba Paschal Serge Wawa ataukosa mchezo wa pili wa robo fainali ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe utakaopigwa Jumamosi, April 13 huko Lubumbashi DR Congo

Wawa alipata majeraha ya kifundo cha mguu kwenye mchezo wa kwanza uliopigwa uwanja wa Taifa ambao ulimalizika kwa suluhu ya bila kufungana

Uongozi wa Simba umethibitisha kuwa Wawa atakaa nje kwa wiki moja

Wawa hatajumuishwa kwenye kikosi cha Simba kitakachoondoka Alfajiri ya kesho kuelekea Lubumbashi