Mazoezi ya mwisho kabla ya kuikabili Kagera Sugar

Kikosi cha Yanga leo kimefanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa CCM Kirumba tayari kwa mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar

Mchezo huo utapigwa kesho Alhamisi katika dimba hilo

Kocha Mkuu wa mabingwa hao wa kihistoria Mwinyi Zahera amesema mazoezi waliyofanya tangu jana yalikuwa ya kuondoa uchovu kwa wachezaji wake

Amesema ana matarajio kuwa vijana wake watakuwa sawa katika mchezo wa kesho baada ya kuwapa mazoezi hayo maalum