Licha ya kutangulia kufunga bao la kuongoza kwenye dakika ya pili kupitia kwa Emmanuel Okwi, Simba ilishindwa kulinda bao hilo huku mfumo wa kujihami zaidi uliotumiwa na kocha Patrick Aussems ukitajwa kuigharimu Simba katika kipindi cha kwanza na kujikuta ikiruhusu mabao mawili mpaka wakati wa mapumziko
TP Mazembe ilitawala zaidi mchezo kwenye kipindi cha pili kwa kutengeneza nafasi nyingi huku ikifanikiwa kutumia nafasi nyingine mbili kujihakikishia ushindi wa mabao 4-1
Licha ya kuondoshwa katika hatua ya robo fainali, mafanikio ya kufika hatua hiyo ni ya kujivunia kwa Simba
Aidha bila shaka Simba itaendeleza hapa ilipoishia kwa kuimarisha zaidi kikosi chake ili kuwa cha ushindani zaidi msimu ujao

