
Simba ina nafasi ya kutinga nusu fainali ya michuano hiyo kama itaibuka na ushindi au kutoka sare yoyote ya mabao
Simba ilitua Lubumbashi mapema jana Ijumaa na jioni kupata nafasi ya kufanya mazoezi katika uwanja wa Mazembe ambao utatumika baadae
Kocha Patrick Aussems amesema kikosi chake kiko tayari kuelekea mchezo huo na amewataka wapenzi, mashabiki wa Simba na Watanzania wote kwa ujumla kuwaombea dua ili waweze kuibuka na ushindi
Ushindi wa Simba leo ni faida kwa Tanzania kwani matokeo hayo yataisaidia Tanzania kuongezewa timu za kushiriki michuano ya CAF kuanzia msimu ujao
Simba tayari imedhihirisha kuwa inaweza kupambana na timu yoyote barani Afrika, mchezo wa leo utadhihirisha mara dufu uimara wa Simba
Kila la kheri Simba, kila la kheri mabingwa wa nchi, kila la kheri wawakilishi wa Tanzania..