Serengeti Boyz kuvuna mamilioni wakishinda michezo miwili AFCON U17

Wachezaji wa timu ya taifa ya vijana ya Tanzania, U-17 ‘Serengeti Boys’ wameahidiwa kupewa Sh. 20 milioni kila mchezaji endapo watashinda michezo miwili katika michuano ya AFCON U17 inayoanza kesho jijini Dar es salaam

Ahadi hiyo imetolewa jana na Mlezi wa timu hiyo Dkt.Reginald Mengi pamoja na Kamati ya kuhamasisha ushindi wa timu hiyo inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar, es salaam, Paul Makonda.

Serengeti Boys inahitaji kushinda mechi mbili ili kujikatia tiketi ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia kwa vijana chini ya miaka 17 itakayofanyika nchini Brazil mwaka huu.

Michuano hiyo itafanyika katika viwanja viwili, ambavyo ni Uwanja wa Taifa na Uwanja wa Azam Complex Chamazi.

Timu shiriki zimepangwa katika makundi mawili, ambapo kundi A lina timu za Tanzania, Nigeria, Angola na Uganda, huku kundi B likiwa na timu za Guinea, Cameroon, Morocco na Senegal.