Ajib mbioni kurejea kikosini Yanga

Nahodha wa Yanga Ibrahim Ajib amekosekana dimbani kwa takribani wiki tatu akisumbuliwa na majeraha ya nyonga

Kinara huyo wa kutengeneza mabao ligi kuu huenda akarejea kikosini kwenye mchezo ujao dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa mkoani Morogoro April 17 2019

Kukosekana kwake katika michezo iliyopita kumeibua maswali mengi miongoni mwa mashabiki wa Yanga hasa baada ya kuibuka tetesi kuwa anataka kurudi katika timu yake ya zamani, Simba

Hata hivyo Msemaji wa Yanga Dismas Ten amesisitiza kuwa Ajib amekosa michezo iliyopita kutokana na kuwa majeruhi na si vinginevyo

Amesema atarejea kikosini baada ya kupona majeraha hayo