
Katika mchezo wa ufunguzi kati ya Serengeti Boyz dhidi ya Nigeria idadi ya mashabiki waliojitokeza hawakuwa wengi hali iliyopelekea Serikali kuchukua uamuzi huo
Michezo yote inayopigwa kuanzia leo haitakuwa na viingilio hivyo Watanzania wameaswa kujitokeza kwa wingi kushuhudia michuano hiyo inayofanyika katika viwanja vya Taifa na Azam Complex