Serikali yafuta viingilio AFCON U17

Wakati wa ufunguzi wa michuano ya AFCON U17 jana, Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa alitangaza kufuta viingilio kwenye michuano hiyo inayofanyika nchini kwa mara ya kwanza

Katika mchezo wa ufunguzi kati ya Serengeti Boyz dhidi ya Nigeria idadi ya mashabiki waliojitokeza hawakuwa wengi hali iliyopelekea Serikali kuchukua uamuzi huo

Michezo yote inayopigwa kuanzia leo haitakuwa na viingilio hivyo Watanzania wameaswa kujitokeza kwa wingi kushuhudia michuano hiyo inayofanyika katika viwanja vya Taifa na Azam Complex