Zahera akerwa na waamuzi ligi kuu

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema kumekuwa na makosa mengi yanafanywa na waamuzi hasa kuionea Yanga lakini anasikitishwa kuona wanaondesha mpira nchini hawachukui hatua yoyote

Zahera aliyazungumza hayo jana baada ya mchezo kati ya Mtibwa Sugar dhidi ya Yanga, mchezo ambao wenyeji waliondoka na ushindi wa bao 1-0

Zahera amesema kwa mfumo huu wa kuzibeba dhahiri baadhi ya timu, ana mashaka na hatma ya mpira wa Tanzania kuwa utaendelea kubaki chini