Tutarekebisha makosa – Ninja

Bekiwa Yanga, Abdallah Shaibu ‘Ninja’, amewataka mashabiki wa timu hiyo kutokuwa na wasiwasi, kwani kikosi chao kitarekebisha makosa na kufanya vizuri.

Ninja amesema hayo siku moja baada ya Yanga kuchapwa bao 1-0 na Mtibwa Sugar, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Ninja amewataka mashabiki wa Yanga kuendelea kuwa wavumilivu, kwani wanapambana kwa ajili ya timu hiyo.

“Naomba mashabiki wetu waendelee kuwa wavumilivu, kwani wenyewe wanaona tunavyopambana na hata wanachotufanyia waamuzi,” Ninja amenukuliwa na Bingwa

Alisema kwa sasa matokeo dhidi ya Mtibwa Sugar wameshayasahau na akili zao wamezielekeza kwenye mchezo unaofuata dhidi ya Azam, ambao utachezwa Aprili 29, mwaka huu.

“Mpira ni mchezo wa makosa, ukifanya kosa moja wenzako wanakuadhibu, ila naamini benchi la ufundi limeona na tutafanyia kazi, ila kikubwa tunaendelea kuvumilia wakati tunazidi kupambana”