Yanga kusaka alama tatu mchezo dhidi ya Prisons leo

Ligi Kuu ya Tanzania Bara inaendelea leo kwa mchezo mmoja kupigwa ambapo vinara wa ligi hiyo Yanga watakuwa uwanja wa Uhuru kuikabili Tanzania Prisons

Yanga inahitaji kushinda mchezo huo ili kuendelea kuipa ‘presha’ Simba kwenye mbio za kuwania ubingwa msimu

Aidha, itakuwa ikisaka rekodi ya kuwa timu kwanza kufikisha alama 80 msimu huu

Wapinzani wao katika mbio za upingwa Simba wao wanaelekea mkoani Mbeya ambapo kesho May 03 watacheza na Mbeya City kisha May 05 watacheza na Tanzania Prisons

Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema wachezaji wote wako katika hali nzuri, tayari kwa mchezo huo utakaopigwa kuanzia saa kumi kamili jioni