Mchezo huo uliathiriwa na mazingira ya uwanja uliojaa maji baada ya mvua kunyesha muda mchache kabla ya mchezo kuanza
Mbeya City ilitangulia kufunga bao katika dakika ya 22 kupitia kwa Iddi Selemani Naddo
Hata hivyo Simba ilirejea ikiwa imara kwenye kipindi cha pili na kusawazisha bao hilo kupitia kwa Jonas Mkude kwenye dakika ya 68 kabla Meddie Kagere hajaihakikishia Simba alama tatu muhimu kwa kufunga bao la ushindi kwenye dakika ya 85

Ushindi huo umeifanya Simba ifikishe alama 75, ikiendelea kushika nafasi ya pili kwa tofauti ya alama tano dhidi ya Yanga
Itacheza mchezo mwingine dhidi ya Tanzania Prisons keshokutwa Jumapili hapohapo dimba la Sokoine