FT : Simba 8-1 Coastal Union

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wamerejea kileleni mwa msimamo wa ligi kibabe baada ya kuifumua Coastal Union mabao 8-1 kwenye mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru

Leo ilikuwa siku ya sherehe ya mabao kwa washambuliaji wawili wa Simba Emmanuel Okwi na Meddie Kagere ambao wamefunga ‘hat-trik’ kila mmoja

Alianza Okwi kupiga hat-trik kabla ya Kagere kupata ya kwake kwenye kipindi cha pili

Mabao mengine mawili yalifungwa na viungo Hassani Dilunga na Clatous Chama aliyefunga bao lake kwenye dakika za majeruhi

Kagere amejichimbia kileleni katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu akiwa amefikisha mabao 201 wakati Okwi amemfikia John Bocco baada ya kufikisha mabao 14

Simba ni kama imezianza sherehe za ubingwa leo na itahitaji kushinda michezo minne tu ili kutawazwa mabingwa kwa msimu wa pili mfululizo