Hatma ya Okwi kujulikana mwishoni mwa msimu

Mshambuliaji hatari wa Simba Emmanuel Okwi amesema hatma yake ya kuendelea kukipiga Msimbazi itafahamika mwishoni mwa msimu mkataba wake utakapokuwa umemalizika kabisa

Okwi amekuwa akihusishwa kutakiwa na klabu za Orlando Pirates na Kaizer Chiefs zinazoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini

Mwishoni mwa mwaka jana klabu ya Kaizer Chiefs ilituma ofa kwa Simba kutaka kumsajili mshambuliaji huyo, ofa ambayo ilikataliwa na uongozi wa mabingwa hao wa Tanzania

Jana baada ya mchezo dhidi ya Coastal Union Okwi aligoma kuweka hadharani hatma yake akibainisha kuwa mazungumzo yatafanyika mwishoni mwa msimu na lolote linaweza kutokea

Uongozi wa Simba tayari umeanza mazungumzo na wachezaji ambao mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu

Mbali na Okwi, wachezaji wengine ambao mikataba yao iko ukingoni ni pamoja na Aishi Manula, John Bocco, Erasto Nyoni, Nicolas Gyan, Shomari Kapombe na Jonas Mkude