Sababu ya Ajib kuachwa Dar yatajwa

Kikosi cha Yanga kiko mkoani Mara ambapo kesho kitashuka katika uwanja wa Karume kuikabili Biashara United katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara

Hata hivyo Yanga ilisafiri bila ya nahodha wake Ibrahim Ajib ambaye aliondolewa kwenye kikosi baada ya kuugua ghafla

Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema Ajib alipata maradhi wakati wakiwa kambini usiku wa kuamkia jana ambapo alipatiwa huduma ya kwanza na Dk Edward Bavu kabla ya kukimbizwa Hospitalini

Hafidh amesema hali ya kiungo huyo kinara wa kutoa pasi za mabao ligi kuu ya Tanzania Bara, inaendelea vizuri

Yanga iliwasili Musoma jana na kupokelewa kwa shangwe na mamia ya mashabiki wa timu hiyo