STARS Kujifua Afrika Kusini Siku 10

Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars” imeondoka leo alfajiri kuelekea nchini Afrika Kusini kuweka Kambi kujiandaa na mchezo wake wa kutafuta tiketi ya kufuzu Afcon 2019 dhidi ya Lesotho.

Kambi hiyo ya siku 10 itakuwa katika Mji wa Bloemfontein kabla ya kikosi hicho kuelekea mjini Maseru,Lesotho.

Taifa Stars ipo nafasi ya pili katika kundi L ikiwa na alama 5 nyuma ya vinara Uganda wenye alama 10 wakati Cape Verde wapo nafasi ya tatu wakiwa na alama 4 na Lesotho wakiburuza mkia na alama mbili.

Mchezo dhidi ya Lesotho unataraji kuchezwa Novemba 18,2018 mchezo ambao utatoa taswira ya Taifa Stars kufuzu kucheza Afcon mwakani itakayofanyika Cameroon.

Leave a comment