Michezo sita ya ligi kuu ya Tanzania Bara mzunguuko wa 14 imepigwa leo katika viwanja mbalimbali.
Alliance Fc imefanikiwa kuibuka na ushindi wa pili mfululizo baada ya kuilaza Mtibwa Sugar bao 1-0.
Baada ya kuchezea vichapo vizito kwenye michezo miwili iliyopita, leo Ruvu Shooting imezinduka na kufanikiwa ‘kuipapasa’ Stand United mabao 2-1
Haya hapa matokeo ya michezo yote iliyopigwa leo;
Ligi hiyo itaendelea kesho Alhamisi kwa mechezo mmoja kupigwa kati ya Mbeya City dhidi ya JKT Tanzania.
Timu za Yanga, Simba na Azam Fc zinaendelea ‘kurundika’ viporo baada ya michezo yao kuahirishwa kutokana na kuwa na wachezaji wengi kwenye timu ya Taifa
