Aussems Ataka Michezo ya Kirafiki SIMBA SC

Ligi Kuu ya Tanzania Bara itasimama kwa wiki mbili baada ya michezo ya leo kupisha michezo ya Kimataifa iliyo katika kalenda za CAF na FIFA.

Kwa upande wa Simba, Yanga na Azam Fc ligi hiyo ilisimama mapema hadi baada ya michezo ya Kimataifa kutokana na kuwa na wachezaji wengi kwenye kikosi cha timu ya Taifa.

Simba ndio iliyoathirika zaidi kwani imetoa wachezaji 12 kwenye timu za Taifa za wakubwa na U23.

Hata hivyo kocha Mkuu wa timu hiyo Patrick Aussems ameendelea kuwafua vijana wake kuwaandaa na michezo ya baada ya michuano ya Kimataifa kupita.

Aussems ameutaka uongozi wa klabu ya Simba umtafutie michezo miwili ya kirafiki ili kuwaweka vijana wake katika hali ya ushindani.

Aussems ambaye kikosi chake kinakabiliwa na mchezo wa ligi ya mabingwa mwishoni mwa mwezi huu, ametaka atafutiwe mchezo wa kirafiki na timu ya hapa nyumbani na mwingine dhidi ya timu kutoka nje ya nchi.

Leave a comment