#ManchesterDerby – Kuelekea mchezo wa Derby ya Jiji la Manchester jumapili hii – tuangalie umuhimu wa Maroune Fellaini ‘Kipenzi cha Jose Mourinho’ katika timu ya United.
:
Fellaini ambaye alikuwa ameumia kwa wiki kadhaa kabla ya kurudi katika mchezo dhidi ya Juventus ambapo alichangia kwa kiasi kikubwa kuirudisha United Uingereza na ushindi vs Juventus.
:
Kocha wa Juventus Massimiliano Allegri alisema hawakuweza kupambana na Fellaini alipoongia – aliwazidi kwenye kucheza mipira ya juu na aliwaletea madhara yaliyoenda kusababisha mashambulizi mengi langoni mwao.
:
Mourinho amekuwa akimzungumzia Fellaini kwa kumuita ‘Plan B’ pindi mipango yake ya mwanzo inapogoma na amekuwa akiisaidia sana United pindi aingiapo dimbani.
:
Takwimu zinaonyesha United inafunga magoli kwa wastani Fellaini anapokuwepo dimbani kuliko ambapo anakuwa hayupo. :
Kuelekea mchezo vs City, United wanamhitaji sana Fellaini awe kwenye kiwango bora kwa maana kiuhalisia United hawawezi kupambana na City kwa kucheza mpira chini – wanahitaji mbinu mbadala na uwepo wa Fellaini kikosini utaongeza ubora wa mbinu ya tofauti ya kuweza kuiletea madhara defence ya City. :
Manchester Derby ya kwanza ya msimu itachezwa jumapili hii majira ya saa 1:30 usiku – itaonyeshwa live kupitia @dstvtanzania pekee