Mzee Akilimali Apinga MANJI Kurudi Yanga

Katibu wa Baraza la Wazee la Yanga Ibrahim Akilimali amepinga kurejea kwa Mwenyekiti wa klabu hiyo Yusufu Manji na ameitilia shaka barua inayodaiwa kuwa ameiandika kuridhia kurejea katika nafasi yake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Akilimali ambaye tayari amechukua fomu ya kugombea nafasi ya Uwenyekiti ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) iichunguze barua hiyo iliyosomwa na Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini Kapteni George Mkuchika.

Aidha Akilimali amedai kushangazwa na viongozi wa Yanga kuendelea kumsemea Manji wakati yeye mwenyewe yupo.

Akilimali amemtaka Manji ajitokeze hadharani kuwaambia WanaYanga kama amerejea au la na sio kusemewa na watu wengine kila siku.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti kamati ya Uchaguzi ya TFF Malange Mchungahela amewataka viongozi wa Baraza la Wadhamini Yanga pamoja na wajumbe Kamati ya Utendaji wajieleze kwanini wasichukuliwe hatua kutokana na kutaka kuvuruga mchakato wa Uchaguzi wa klabu hiyo.

Mchungahela amesisitiza kuwa zoezi la utolewaji wa fomu kwa ajili ya nafasi zote za uchaguzi zilizotangazwa (ikiwemo ya Mwenyekiti) linaendekea na litafikia tamati 14/11/2018.

Amesema wale wanaomtaka Manji arejee Yanga basi ni vyema wakaenda kumchukulia fomu

Leave a comment