Simba vs Big Bullet Haji Manara Aweka wazi Viingilio

Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Simba keshokutwa Ijumaa, Novemba 16 2018 watashuka kwenye uwanja wa Taifa kuwakabili mabingwa wenzao Nyasa Big bullets kutoka nchini Malawi katika mchezo wa kirafiki.

Mchezo huo wa Kimataifa wa kirafiki unatarajiwa kuanza saa 12 jioni.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo, Afisa Habari wa Simba Haji Manara amesema watautumia mchezo huo kama sehemu ya maandalizi ya kikosi chao kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Mbabane Swallows utakaopigwa Novemba 27.

Manara ametaja viingilio vya mchezo huo kuwa ni;
VIP A : 10,000/-
VIP B na C : 7,000/-
Mzunguuko : 3,000/-

Manara amewataka mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa keshokutwa ili kuiunga mkono timu yao.