Vijana wa STARS wanacheza na Burundi

Leo Jumatano saa 10 jioni kikosi cha timu ya Taifa ya vijana umri chini ya miaka 23, kinashuka kwenye uwanja wa Prince Louis Rwagasore kuwakabili wenyeji wao Burundi katika mchezo wa kusaka tiketi ya kutinga fainali za AFCON 2019 kwa vijana.

Stars U23 ilisafiri na kutua Burundi jana ambapo jioni ilifanya mazoezi ya mwisho kuelekea mchezo huo utakaopigwa saa kumi jioni.

Kikosi cha Stars U23 kilichokwenda Burundi kilijumuisha wachezaji 20, na viongozi wa benchi la ufundi.

Mlinda lango Ramadhani Kabwili na beki Abdallah Shaibu ‘Ninja’ kutoka klabu ya Yanga ni miongoni mwa wachezaji waliojumuishwa kwenye kikosi hicho