Mabingwa wa kihistoria wa Tanzania, Yanga leo wanashuka kwenye uwanja wa Uhuru kuikabili Reha Fc katika mchezo wa kirafiki kwa ajili ya kukiandaa kikosi hicho.
Huo unakuwa mchezo wa pili kwa Yanga kipindi hiki ambacho ligi imesimama kupisha michuano ya Kimataifa. Jumapili iliyopita iliilaza African Lyon bao 1-0.
Ni kwa Tsh 5,000/- tu utaushuhudia mchezo huo ukiwa umekaa majukwaa ya VIP wakati kule upande wa mzunguuko ni Tsh 3,000/-